Ujerumani: Wanane wauawa katika mashambulizi ya risasi karibu na Frankfurt
Maafisa wa usalama nchini Ujerumani, wanaendelea na msako mkubwa, kuwatafuta watu waliotekeleza mashmabulizi mawili ambayo yamesababisha vifo vya watu wanane.
Imechapishwa:
Mashambulizi bayo yametokea katika vilabu viwili vya kuvuta shisha katika eneo la Hanau, karibu Kilomita 20 kutoka mji wa Frankfirt.
Muda mfupi baada ya mashambulizi hayo, polisi wameonekana katika eneo la tukio, huku wengine wakitumia helikopta kuwasaka waliohusika.
Shambulizi la kwanza, lilitokea saa nne usiku siku ya Jumatano, baada ya mtu aliyekuwa na silaha kuwauwa watu watoto katika kilabu ya moja na baadaye kwenda katika eneo lingine na kuwauwa watu watano akiwemo mwanamke mmoja.
Haijafahamika iwapo, mashambulizi hayo yalitekelezwa na mtu mmoja au watu wengi, na lengo la mauaji haya, halijafahamika.