Waziri Mkuu Theresa May huenda akatangaza ni lini atajiuzulu
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May anatarajiwa kutangaza tarehe ya kujiuzulu kwake siku ya Ijumaa, chanzo kimoja kutoka bungeni kimeliambia Shrika la Habari la Uingereza BBC.
Imechapishwa:
Bunge linataraji Waziri Mkuu huyo kutaja ratiba ya mrithi wake kuchaguliwa, kuelekea tarehe 10 mwezi Juni ambapo huenda ikawa tarehe rasmi ya kuanza mbio za uongozi.
Bi.May anatarajiwa kukutana na Mwenyekiti wa chama chake cha Conservative kujadili juu ya hatma yake huku tayari kuna idadi kadhaa ya viongozi wa chama cha Conservative ambao wako njiani kuwania wadhifa wa Waziri Mkuu May.
May yumo katika shinikizo kubwa kutaja tarehe ambayo ataondoka madarakani baada ya juhudi zake za mwisho za mpango wa kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya, yaani Brexit kushindwa,
Tangu mwezi Januari bunge lilikataa mkataba wa kujitoa kati ya Theresa May na EU kwa mara tatu na majaribio ya hivi karibuni kupata muafaka wa pamoja na chama cha Labour kushindwa.