Mbunge mmoja ajeruhiwa vibaya Uingereza
Mbunge mmoja anayetetea Uingereza kubaki katika Umoja wa Ulaya nchini Uingereza, Jo Cox amejeruhiwa kwa risasi Alhamisi hii, huku akichomwa kisu na mshambuliaji mwenye umri wa miaka 52.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Kampeni dhidi ya kuondoka au la kwa Uingereza katika Umoja wa Ulaya imesimamishwa baada ya tukio hilo.
Jo Cox, Mbunge kutoka Uingereza, mwenye umri wa miaka 41, anaunga mkono Uingereza kubaki katika Umoja wa Ulaya. Amejeruhiwa kwa risasi wakati alipokua akikutana na wafuasi wake katika jimbo lake. Baada ya kupigwa risasi, Jo Cox alidondoka kati ya magari mawili madogo madogo, mmoja wa mashahidi amesema.
Jo Cox aliingilia kati wakati watu wawili walikua wakipigana. Jo Cox alisafirishwa hospitali akiwa katika hali mbaya, kaskazini mwa nchi. Mtu mwingine alipata majeraha madogo.
Waziri Mkuu "atiwa wasiwasi"
Shambulizi hili limetokea wiki moja kabla ya kura ya maoni juu kuondoka au la kwa Uingereza katika Umoja wa Ulaya. Kufuatia kitendo hicho, kampeni dhidi ya kuondoka kwa Uingereza katika Umoja wa Ulaya imesimamishwa. Kwenye Twitter, David Cameron, Waziri Mkuu wa Uingereza, amesema anatiwa "wasiwasi", akiongeza kuwa "katika mawazo yetu na sala zetu tuko pamoja na Jo na familia yake."
Very concerned about reports Jo Cox has been injured. Our thoughts and prayers are with Jo and her family.
— David Cameron (@David_Cameron) June 16, 2016
Kiongozi wa chama cha Labour, Jeremy Corbin amesema "anahuzunishwa na kisa hicho."
Jo Cox, aliyechaguliwa tangu mwaka 2015, anaolewa na Breendan Cox, mshauri wa zamani wa Gordon Brown, Waziri Mkuu wa zamani.