Pata taarifa kuu
UFARANSA-ARGENTINA-AJALI-USALAMA

Watu 10 wamefariki katika ajali ya helikopta Argentina

Watu kumi ikiwa ni pamoja na raia wanane wa Ufaransa wamefariki katika ajali ya helikopta iliyotokea katika mkoa wa La Rioja, nchini Argentina.

Kijiji cha Villa Castelli, mkoa wa La Rioja, Machi 9 mwaka 2015.
Kijiji cha Villa Castelli, mkoa wa La Rioja, Machi 9 mwaka 2015. AFP PHOTO / ALDO PORTUGAL
Matangazo ya kibiashara

Miongoni mwa waliofariki ni pamoja na Florence Arthaud, bingwa wa michezo ya kuogelea ya olimpiki Camille Muffat na mwanamisumbi Alexis Vastine.

Mabingwa hao watatu wamekua wakishiriki pamoja na wanariadha wengine wa Ufaransa katika utengenezaji wa makala ya " télé-réalité", ambayo ni mchezo mpya wa kusisimua wa televisheni ya Ufaransa TF1.

Watu wote hao kumi waliofariki walikua katika helikopta mbili walizokua wakitumia katika kazi yao hio, ambazo ziligongana, kwa mujibu wa viongozi wa mkoa wa La Rioja.

Kwa mujibu wa mwandishi wa RFI, katika mji wa Buenos Aires, Jean-Louis Buchet, ajali hiyo imetokea saa kumi na moja jioni saa za Argentina (sawa na saa mbili usikusaa za kimataifa), katika mkoa wa La Rioja, kwenye umbali wa kilomita 2000 kaskazini magharibi mwa mji mkuu wa Argentina, Buenos Aires. Helikopta hizo zilikua zikitokea katika kijiji cha Villa Castelli, katika eneo la Andes.

Inaarifiwa kua helikopta hizo ziligongana baada ya kuruka kwenda juu kwenye umbali wa mita 100. Picha za ajali hiyo zinatisha.

Saa moja baadae, polisi ya moka wa La Rioja ilitoa taafa kwamba hakuna mtu aliyenusurika katika ajali hiyo. Marubani wawili kutoka Argentina wote wamefariki.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.