Pata taarifa kuu

Miezi 7 yaongezwa katika mazungumzo kati ya Iran na nchi zenye nguvu

Nchi ya Iran na mataifa yenye nguvu duniani yameshindwa kufikia muafaka katika siku ya mwisho Jumatatu Novemba 24 kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.

Hassan Rohani anahitaji kuendelea kwa mazungumzo ili kuepuka kukosolewa na mahasimu wake Waconservative
Hassan Rohani anahitaji kuendelea kwa mazungumzo ili kuepuka kukosolewa na mahasimu wake Waconservative REUTERS/president.ir/Handout
Matangazo ya kibiashara

Nchi hizo sita pamoja na Iran zimekubaliana kuongeza miezi mingine saba ya mazungumzo kati yao.

Kushindwa kufikiwa kwa makubaliano hayo siku ya Jumatatu, kumefuatia mazungumzo ya kina yaliyofanyika kwa zaidi ya siku tano mjini Vienna, Austria kati ya ujumbe wa Iran, Marekani, Urusi, China, Uingereza, Ufaransa pamoja na Ujerumani.

Kwa upande wake waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani, John Kerry amesema kuwa licha ya kutofikiwa muafaka lakini walau wamepiga hatua kwenye mazungumzo yao.

Kauli ya waziri Kerry iliungwa mkono na waziri mwenzake wa mambo ya kigeni wa Uingereza, Philip Hammond ambaye amesema licha ya kupiga hatua kwenye mazungumzo hayo changamoto bado ni kubwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.