Pata taarifa kuu
MAREKANI-QATAR-TALIBAN

Makubaliano kati ya Marekani na Taliban ya kubadilishana wafungwa, yahojiwa

Hatau ya kundi la Taliban, Qatar na nchi ya Marekani kufukia makubaliano kwa kubadilishana wafungwa hao wa Taliba kwa mwanajeshi mmoja wa Marekani aliyikuwa anashikiliwa kwa zaidi ya miaka mitano na kundi hilo, imeibua maswali kuhusu sera ya Qatar na kundi la Taliban.Β 

Le sergent Bowe Bergdahl, capturΓ© par les talibans le 30 juin 2009,  Γ©tait apparu sur une vidΓ©o du groupe Manba al-Jihad le 7 dΓ©cembre 2010. Il Γ©tait le seul prisonnier de guerre amΓ©ricain en treize ans de guerre en Afghanistan.
Le sergent Bowe Bergdahl, capturΓ© par les talibans le 30 juin 2009, Γ©tait apparu sur une vidΓ©o du groupe Manba al-Jihad le 7 dΓ©cembre 2010. Il Γ©tait le seul prisonnier de guerre amΓ©ricain en treize ans de guerre en Afghanistan. AFP PHOTO HANDOUT-INTELCENTER"
Matangazo ya kibiashara

Serikali ya Marekani imesema kuwa tayari wamempokea mwanajeshi wao, Sajenti Bowe Bergdahl ambaye alisafirishwa hadi nchini Ujerumani kwenye hospitali ya jeshi la Marekani kwa uchunguzi zaidi wa kiafya.

Wapiganaji wa Taliban
Wapiganaji wa Taliban REUTERS

Uamuzi huu wa kubadilishana wafungwa wa Taliban na mwanajeshi wa Marekani, ilisimamiwa na nchi ya Qatar ambayo imesema makubaliano haya yalitokana na sera yake ya kuheshimu haki za binadamu bila kutoa ufafanuzi zaidi.

Akizungumza saa chache baada ya mwanajeshi huyo kuachiliwa, rais Barack Obama akiwa na wazazi wa mwanajeshi huyo kwenye ikulu ya Washington, amesema kuwa Bowe alikosa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa na mapumziko na kwamba Serikali yake haikufanya vyakutosha kuhakikisha anaachiliwa huru.

Rais Obama ametoa pongezi kwa mfalme wa Qatar, Sheikh Tamim bin Hamad Al-Thani pamoja na utawala wa Kabul kwa kuhusika moja kwa moja katika kuhakikisha mwanajeshi hiyo anaachiwa huru.

Rais wa Marekani, Barack Obama akiwa na wazazi wa mwanajeshi aliyeachiwa huru na wapiganaji wa Taliban
Rais wa Marekani, Barack Obama akiwa na wazazi wa mwanajeshi aliyeachiwa huru na wapiganaji wa Taliban USgvt

Serikali ya Qatar hapo jana wakati ikijibu maswali ya waandishi wa habari, ilikataa katukatu kuweka wazi misingi ya kuachiwa kwa viongozi hao wa Taliban ambao walikamatwa wakati wa vita ya kulisambaratisha kundi hilo nchini Afghanistan.

Hatua hii imeibusha maswali mengi toka kwa wanaharakati ambao wanadai kuwa huenda viongozi hao wakarejea uraiani na kuanza tena harakati zao za kuipinga Serikali ya Afghanistan.

Utawala wa Qatar umesema kuwa licha ya viongozi hao kuachiwa huru, kuna hatua ambazo wao watazichukua kama nchi kuhakikisha hawarejei kwenye harakati zao na kundi la Taliban.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.