Serikali ya Venezuela yataka kuvunja Bunge
Serikali ya Venezuela inapanga kuomba Mahakama Kuu (TSJ) kuvunja Bunge, ambalo kwa sasa linadhibitiwa na upinzani, kwa kuingilia kazi za serikali, msemaji wa muungano wa vyama vinavyoshiriki katika serikali, Didalco Bolivar, amesema Jumanne hii.
Imechapishwa:
Kambi ya Rais Nicolas Maduro kutoka chama cha Kisoshalisti "imeanzisha majadiliano" kabla ya kuwasilisha ombi lake kwa kitengo cha Katiba cha Mahakama Kuu (TSJ) na kuomba "kuvunjwa kwa Bunge" hilo, ambapo wabunge kutoka chama cha mrengo wa kati ni wengi tangu mwezi Januari, Bw Bolivar amesema katika mkutano na waandishi wa habari.
Katikati ya mwezi Juni, Mahakama Kuu, inayoshtumiwa na upinzani kuegemea upande wa serikali ilishatoa jibu lake linalounga mkono mashtaka ya Rais Maduro kwa kuingilia kazi za serikali, na kusababisha kufutwa kwa maamuzi mawili yalikua yalichukuliwa na Bunge linalotawaliwa na upinzani.
Serikali na Bunge wameendelea kuvutana kwa miezi kadhaa, huku upinzani kutafuta kuondoka kwa haraka kwa Nicolas Maduro, aliyechaguliwa mwaka 2013 hadi 2019, kupitia kura ya maoni.
Mapambano haya utawala yanakuja katika mazingira ya mgogoro mkubwa wa kiuchumi kwa nchi hii yenye utajiri wa mafuta inayokabiliwa na kushuka kwa bei mafuta ghafi, inayosababishwa na upungufu wa chakula na madawa na hivyo kuibua maandamano zaidi ya kijamii.
Mbali na mashitaka ya kuingilia kazi za serikali, serikali ya muungano inapanga, katika ombi lake itakalowasilisha kwa Mahakama Kuu, mashitaka ya uhaini, ukiukwaji wa Katiba na matumizi mabaya ya mamlaka katika masuala ya sera za kigeni.
"Tunatoa wito kwa ajili ya kuvunjwa (ya Bunge) ni akiongozana na wito kwa ajili ya uchaguzi iwapo watu wanaosema kwamba kama hii Assembly ni filibustering na linakiuka Katiba lazima kuweka" au la, alisema Didalco Bolivar.
Majadiliano kuhusu uwezekano wa kufungua mashitaka mbele ya Mahakama Kuu yameanza Jumanne hii na uamuzi utatangazwa wiki ijayo, Didalco Bolivar ameongeza.