Pata taarifa kuu
Gurudumu la Uchumi

Afrika inajifunza nini kuhusu ukuaji wa uchumi wa taifa la Nigeria.

Imechapishwa:

Juma hili kwenye makala ya Gurudumu la Uchumi, tumeangazia sehemu ya pili ya namna ambavyo nchi ya Nigeria imefanikiwa katika kuimarisha uchumi wake kupitia sekta mbalimbali ambazo awali hazikujumuishwa kwenye ukokotoaji wake.

Msanii D'Banji akiwa na wasanii wengine nchini Nigeria ambao wamechangia kwa sehemu kubwa ukuaji wa sekta ya uchumi
Msanii D'Banji akiwa na wasanii wengine nchini Nigeria ambao wamechangia kwa sehemu kubwa ukuaji wa sekta ya uchumi ONE France
Matangazo ya kibiashara

Mtangazaji wa makala hii, amezungumza na mtaalamu wa masuala ya Uchumi wa dunia, Daktari Honesty Ngowi ambaye pia ni mhadhiri kwenye chuo kikuu cha mzumbe nchini Tanzania.

RFI/Dandago

Dr Ngowi anajaribu kueleza ni kwanini Nigeria uchumi wake umekua kwa haraka na kuelezwa kuwa miongoni mwa mataifa ambayo sasa ni tishio kiuchumi barani Afrika hali ambayo hata imeifanya nchi ya Afrika Kusini Kugutuka.

Mtaalamu huyu ameenda mbali zaidi kwa kueleza pia ni kwanini pamoja na nchi ya Nigeria kukua kiuchumi bado kiuhalisia haijaendelea kama nchi nyingine na hii anasema ni kutokana na kukithiri kwa vitendo vya rushwa nchini humo.

Vipindi vingine
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.