Wachezaji wanaohusishwa na ligi ya Saudi Arabia
NAIROBI – Luka Modric na Hugo Lloris ni miongoni mwa wachezaji kumi wanaohusishwa na ligi ya Saudi Arabia wakiongozwa na Lionel Messi na Karim Benzema, watu wa karibu na mazungumzo yanayowalenga wachezaji hao wamethibitisha.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Sergio Ramos, Jordi Alba, Sergio Busquets, N'Golo Kante, Angel Di Maria na Roberto Firmino pia wametajwa kuwa miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na ligi hiyo.
Taarifa hii inakuja wakati huu maofisa wa ligi hiyo ya Saudi wakiwa mjini Paris na Madrid kujaribu kumaliza mikataba ya Messi na Benzema kwa ujumla, hatua ambayo itawaruhu kujiunga na Cristiano Ronaldo katika ufalme huo wenye utajiri wa mafuta.
Mamlaka ya Saudi ipo katika mawasiliano na zaidi ya wachezaji kumi wengi wao wakiwa ni wale walioshinda kombe la dunia na klabu bingwa barani Ulaya wakitarajiwa kujiunga na ligi ya Saudi msimu ujao.
Kando na Messi, orodha hiyo inajumuisha wachezaji kama vile Benzema, Ramos, Di Maria, Modric, Hugo Loris, Kante, Firmino, Alba na Busquets.
Licha ya kwamba wachezaji hao wamedaiwa kupewa mikataba mikubwa, watacheza katika ligi yenye ushindani mkubwa, Saudi Arabia inalenga kukamilisha uhamisho wao kabla ya msimu mpya wa ligi kuaanza tarehe 11 ya mwezi Agosti.
Kando na watu wa karibu na mazungmzo yanayodaiwa kuwa yanaendelea, afisa wa serikali ya saudi ameiambia AFP kuwa mamlaka inafanya mazungumzo na wachezaji wa tajiriba ya juu.
Kwa mujibu wa mamlaka ya saudi, hatua hii inalenga kuifanya ligi yao kuwa yenye ushindani mkubwa.