AFCON 2021-CAMEROON-SOKA
AFCON: Matumaini ya Zimbabwe kusonga mbele yadidimia
Zimbabwe haina matumaini ya kusonga mbele katika michuano ya mataifa ya Afrika baada ya kufungwa mechi zote mbili za kundi B.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mechi ya kwanza, ilifugwa na Senegal 1-0, kupitia mkwaju wa penalti iliyofungwa na mshambuliaji Sadio Mane.
Mechi ya pili, ilishangazwa na Malawi iliyoicharaza mabao 2-1 matokeo ambayo yanaiacha katika kundi hilo bila ya alama yoyote.
Kundi hili linaongozwa na Guinea ambayo ina alama nne sawa na Senegal, na Malawi ina alama tatu.
Matokeo ya kundi B
Senegal 1-0 Zimbabwe
Guinea 1-0 Malawi
Senegal 0-0 Guinea
Malawi 2-1 Zimbabwe.
Michuano ya mwisho-Januari 18 2022
Malawi vs Senegal
Zimbabwe vs Guinea.