Pata taarifa kuu
MICHEZO YA OLIMPIKI- UGANDA

Kikosi cha Uganda chawekwa karatini kuelekea michezo ya Olimpiki

Kikosi cha kwanza cha timu kutoka nchini, kilichokuwa kimewasili jijini Tokyo nchini Japan Jumamosi iliyopita kushiriki kwenye michezo ya Olimpiki inayoanza Julai 23, wamewekwa karatini baada ya mmoja wa makocha wao kupatikana na virusi vya Corona.

Nembo ya michezo ya Olimpiki nchini Japan
Nembo ya michezo ya Olimpiki nchini Japan REUTERS - ISSEI KATO
Matangazo ya kibiashara

Ripoti zinasema kuwa, kocha huyo ambaye hakutajwa alipatikana na virusi hivyo, licha ya kupokea chanjo kamili ya kuzuia maambukizi hayo aina ya Astra Zeneca kabla ya kuanza safari  nchini Uganda, hakuwa na maambukizi hayo.

Kikosi hicho wa watu 10 sasa kitasalia kwenye Karatini katika hoteli yao mjini Osaka mpaka Julai 3.

Miongoni mwa wachezaji walio kwenye kikosi hicho cha kwanza, ni wale wanaoshiriki kwenye mashindano ya ngumi na maafisa wa juu wa Kamati ya Olimpiki nchini Uganda.

 

Mashindano ya Olimpiki yaliahirishwa kutoka mwaka 2020 mpaka mwaka 2021 baada ya kuzuka kwa janga la Covid 19 na serikali ya Japan, imekuwa ikisema haitawaruhusu mashabiki wa kigeni kuja kushuhudia mashindano hayo. Mashabiki wa ndani 10,0000 ndio wanoatarajiwa kuruhusiwa uwanjani.

Maelfu ya wachezaji kutoka mataifa mbalimbali duniani watakaoshiriki kwenye michezo hiyo, wametakiwa kupata chanjo ya kuzuia maambukizi ya Corona na hawataruhusiwa kutangamana na watu jijini Tokyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.