Pata taarifa kuu
SOKA-EURO 2020

Mabingwa wa zamani kuanza kusaka ubingwa wa soka barani Ulaya

Mechi za kundi ngumu la F, kuwania taji la soka barani Ulaya zinachezwa siku ya Jumanne.

Mchezaji wa Uhispani Alvaro Morata alikosa nafasi nyingi za kufunga mabao katika mechi dhidi ya Sweden Juni 15 2021
Mchezaji wa Uhispani Alvaro Morata alikosa nafasi nyingi za kufunga mabao katika mechi dhidi ya Sweden Juni 15 2021 PIERRE-PHILIPPE MARCOU POOL/AFP
Matangazo ya kibiashara

Mabingwa watetezi Ureno watafungua dimba dhidi ya Hungary, huku mabingwa mabingwa wa zamani, Ufaransa na Ujerumani wakipangwa kukutana katika mechi ya pili.

Siku ya Jumatatu usiku, katika mechi za kundi E, Slovakia walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Poland, huku Uhispania na Sweden zikimaliza mchuano wao bila kufungana.

Slovakia wanaongoza kundi lao kwa alama tatu, huku Uhispania na Sweden zikiwa na alama moja. Poland haina alama yoyote mpaka sasa.

Mechi moja ya kundi D pia ilichezwa Jumatatu usiku, baada ya Jamhuri ya Czech kupata ushindi wa mabao 2-0.

Kundi la D linaongozwa na Jamhuri ya Czech ambayo ina alama tatu, sawa na Uingereza.

Croatia na Scotland, hazina alama yoyote.

Ratiba, Jumatano Juni 16 2021

Finland vs Urusi

Uturuki vs Wales

Italia vs Uswizi

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.