Timu ya Nkana yabanwa mbavu nyumbani michuano ya CAF
Matumainiya timu ya Nkana ya nchini Zambia kufuzu katika ya hatua ya makundi kwenye mashindano ya ligi ya Mabingwa barani Afrika CAF yamezama baada ya kujikuta ikibanwa mbavu nyumbani jana Jumamosi na timu ya Zamalek ya Misri.
Imechapishwa:
Timu hiyo bingwa mara tano wa michuano ya ligi ya mabingwa Afrika ilijikuta ikilazimika kwenda sare tasa na watani wake wa jadi timu ya Zamalek kwenye dimba la Nkana huko Kitwe.
Hii ni mara ya tatu mfululizo ambapo timu ya Nkana inakutana na Zamalek na kumalizika kwa msuguano ingawa mara zote Wamisri wameibuka washindi katika mechi zao za nyumbani na kusonga mbele dhidi ya wapinzani wao Zambia.
Jana Jumamosi, Nkana ilianza kwa kutawala mchezo na kuiwekea shinikizo timu ya Zamalek lakini hata hivyo timu hizo zikaambuia sare tasa.