Drogber na Anelka huenda wakauzwa na klabu ya Shanghai 'Shenhua
Hatima ya Wacheza kandanda nyota kutoka klabu ya Chelsea Didier Drogba na Nicolas Anelka ambao wanachezea klabu ya Shanghai Shenshua huenda ikatumbukia nyongo na wakawa wamecheza mechi ya mwisho kwa klabu ya hiyo ya Shenhua, taarifa zimebainisha jumatano.
Imechapishwa:
Taarifa zimebainisha kuwa mkuu wa klabu ya Shenhua,bilionea Zhu Jun ametishia kusitisha malipo ya wachezaji hao wa kimataifa kufuatia mgogoro uliopo baina ya wanahisa.
Mmoja kati ya viongozi wa klabu hiyo amenukuliwa akisema kama Zhu Jun hatoweza kuungwa mkono na wanahisa wengine atakachofanya ni kuwalipa wachezaji hao kwa kadri aonavyo yeye.
Kiongozi huyo alikaririwa akisema kuwa bado haijulikani kama Drogber atacheza mechi itakayofanyika September 15 au la,jambo ambalo limezua maswali na kuwashangaza wadau na mashabiki wa kandanda ulimwenguni.