Roberto Mancini aonesha matumaini ya kunyakua Kombe la michuano ya ligi kuu Uingereza
Kocha wa Manchester City, Roberto Mancini ana matumaini makubwa kuwa watakuwa mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza, lakini amesema kuwa mechi tatu walizozibakiza zitathibitisha nafasi yao katika ligi hiyo.
Imechapishwa:
Manchester City ilipoteza mchezo baada ya kufungwa bao 1 kwa 0 na Swansea siku ya jumapili, huku Manchester United ikiwa juu yao baada ya ushindi wa mabao 2 kwa 0 dhidi ya West Bromwich Albion.
Ingawa Mancini amekiri kuwa na wakati mgumu,amesema hiyo ndio namna mashindano ya Mpira yalivyo lakini ameonesha kuwa ana uhakika wa kupata taji la kwanza ndani ya miaka 44.
Mancini amesema ingawa wako nyuma ya Manchester United, lengo lao la ushindi halijabadilika wakati huu wakiwa wamebakiza michezo 10.