Pata taarifa kuu

Maofisa wa jeshi la Iran wauuawa katika shambulio la Israeli

Nairobi – Iran imethibitisha kuuawa kwa maofisa wake kadhaa wa jeshi akiwemo kamanda wa juu kwenye jeshi lake, katika shambulio la Israel lililotekelezwa kulenga jengo lililo jirani na ubalozi wake mjini Damascus, Syria.

Israel haijasema chochote kuhusiana na shambulio hilo wala kuthibitisha ikiwa lilikuwa mahsusi kuwalenga maofisa hao
Israel haijasema chochote kuhusiana na shambulio hilo wala kuthibitisha ikiwa lilikuwa mahsusi kuwalenga maofisa hao REUTERS - Firas Makdesi
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa maofisa wa Iran, watu 7 waliuawa katika shambulio hilo ambalo inasema litajibiwa kwa nguvu zote, tangazo linalotishia kuzuka kwa mzozo mwingine kwenye eneo la mashariki ya kati.

Iran imewataja maofisa wake wajuu waliouawa kuwa ni Brigedia Jenerali Mohammed Reza na Brigedia Mohammed Hadi haji, ambao walikuwa wanaongoza vikosi vya kijeshi vinavyofanya operesheni zake Syria, Lebanon na Palestina.

Urusi imelaani shambulio ikisema ni kitendo ambacho hakikubaliki.
Urusi imelaani shambulio ikisema ni kitendo ambacho hakikubaliki. © Omar Sanadiki / AP

Israel haijasema chochote kuhusiana na shambulio hilo wala kuthibitisha ikiwa lilikuwa mahsusi kuwalenga maofisa hao, tukio ambalo mshirika wake wa karibu Marekani, naye amekuwa kimya ingawa imekiri kufahamu kilichotokea.

Katika hatua nyingine wizara ya mambo ya nje ya Urusi, imetoa taarifa kukashifu shambulio hilo ililosema halikubaliki.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.