Pata taarifa kuu

Wanajeshi wa Israeli wameondoka katika hospitali ya Al-Shifa huko Gaza

Nairobi – Wanajeshi wa Israeli wameondoka kwenye eneo la Hospitali ya Al-Shifa, Kaskazini mwa Gaza, baada ya wiki mbili ya operesheni kuwasaka wapiganaji wa Hamas, walioshtumiwa kutumia hospitali hiyo kama kituo cha Makanda wake.

Wanajeshi wa Israeli wamekuwa wakisema wanatekeleza oparesheni kwenye eneo hilo kuwasaka wapiganaji wa Hamas.
Wanajeshi wa Israeli wamekuwa wakisema wanatekeleza oparesheni kwenye eneo hilo kuwasaka wapiganaji wa Hamas. AP - Victor R. Caivano
Matangazo ya kibiashara

Kabla ya kuondoka, Jeshi la Israeli limesema, limewauwa wapiganaji 200 wa Hamas kupitia operesheni yake ya ardhini na angani huku likiwakamata na kuwazuia washukiwa wengine zaidi ya 500  wa kundi hilo.

Aidha, limesema mbali na mauaji, limefanikiwa kunasa kiwango kikubwa cha silaha, vikiwemo vilipuzi pamoja na hela kutoka kwa Hamas.

Wizara ya afya kwenye ukanda wa Gaza, imesema licha ya kuondoka kwa wanajeshi wa Israeli, wameacha uharibifu mkubwa wa miundo mbinu ya hospitali.

Utawala wa Gaza unasema wanajeshi hao walitekeleza ukiukaji wa haki za binadamu kwenye eneo hilo.
Utawala wa Gaza unasema wanajeshi hao walitekeleza ukiukaji wa haki za binadamu kwenye eneo hilo. AFP - -

Wakati wa operesheni hiyo, wagonjwa kadhaa waliuawa na miili yao imekuwa ikizagaa huku miili mingine zaidi ya 20 ikipatikana baada ya kukayangwa na magari ya kijeshi ya Israeli kwa mujibu wa madaktari wa hospitali hiyo.

Baada ya hatua ya Israeli kuondoa vikosi vyake, kundi la Hamas linaitaka Mahakama ya Kimataifa ya ICC kuchunguza mauaji na visa vingine vya uhalifu vilivyofanyika kwenye hospitali ya Al Shifa huku wakiongeza kuwa wanaiwajibisha serikali ya Marekani na rais wake Joe Biden kwa mauaji yaliyotokea kwenye ukanda Gaza.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.