Pata taarifa kuu

Gaza: Israeli yatoa mpango wake baada ya vita kukamilika

Naiorbi – Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant, ametangaza mapendekezo ya utawala wa ukanda wa Gaza, baada ya kumalizika kwa vita kati jeshi la nchi yake na kundi la Hamas.

Kuhusu usalama, ukanda wote wa Gaza utakuwa chini ya Jeshi la Israeli, na kundi la Hamas halitaruhusiwa kuwepo
Kuhusu usalama, ukanda wote wa Gaza utakuwa chini ya Jeshi la Israeli, na kundi la Hamas halitaruhusiwa kuwepo via REUTERS - ISRAEL DEFENSE FORCES
Matangazo ya kibiashara

Miongoni mwa mipango inayowekwa na Israeli ni kuhakikisha kuwa, Gaza inaongozwa kwa kiwango kidogo na Wapalestina.

Kuhusu usalama, ukanda wote wa Gaza utakuwa chini ya Jeshi la Israeli, na kundi la Hamas halitaruhusiwa kuwepo.

Israeli imekuwa ikiendelea na mashambulio katika Ukanda wa Gaza ikisema kuwa inawasaka wapiganaji wa Hamas
Israeli imekuwa ikiendelea na mashambulio katika Ukanda wa Gaza ikisema kuwa inawasaka wapiganaji wa Hamas AP - Mohammed Hajjar

Mapendekezo haya yanakuja, wakati huu jeshi la Israeli likiendeleza mashambulio ambayo kwa saa 24 zilizopita, mauaji ya watu yameendelea kushuhudiwa.

Wizara ya afya kwenye ukanda wa Gaza inasema watu 125 wameuawa kwa kipindi cha saa 24 zilizopita, wakati huu jeshi la Israeli likiapa kuendelea na operesheni dhidi ya kundi la Hamas katika vita ambavyo vimesbabisha vifo vya zaidia ya watu Elfu 22 mpaka sasa.

People carrying some of their belongings arrive in Rafah on the southern Gaza Strip on January 4, 2024, after fleeing from Khan Yunis amid continuing battles between Israel and the Palestinian militan
Mamia ya raia wa Gaza wametoroka katika eneo hilo kwa kuhofiwa kushambuliwa AFP - -

Vita vinaendelea wakati Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken anapotarajiwa kurejea kwenye ukanda huo ambapo atakutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Israeli na Palestina.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.