Pata taarifa kuu

Jeshi la Israel ladai kugundua 'handaki kubwa zaidi' lililochimbwa chini ya Ukanda wa Gaza

Jeshi la Israel limedai siku ya Jumapili kuwa limegundua wakati wa mashambulizi yake "handaki kubwa zaidi" ambalo Hamas imechimba chini ya Ukanda wa Gaza na liko mita mia chache tu kutoka ardhi ya Israel. Mpiga picha wa shirka la habari la AFP ambaye ameidhinishwa kwenda katika eneo hilo amebainisha kuwa handaki hilo ni la ukubwa wa kutosha ambapo magari madogo yanaweza kupita.

Katika picha hii iliyopigwa wakati wa ziara ya vyombo vya habari iliyoandaliwa na jeshi la Israel mnamo Desemba 15, 2023, wanajeshi walitembelea handaki ambalo Hamas inadaiwa kutumia kushambulia Israeli kupitia kivuko cha mpaka cha Erez mnamo Oktoba 7. Jeshi la Israel limesema mnamo Desemba 17, 2023 kwamba limegundua handaki kubwa zaidi la Hamas katika Ukanda wa Gaza hadi sasa, mita mia chache tu kutoka kwenye kivuko cha mpaka cha Erez.
Katika picha hii iliyopigwa wakati wa ziara ya vyombo vya habari iliyoandaliwa na jeshi la Israel mnamo Desemba 15, 2023, wanajeshi walitembelea handaki ambalo Hamas inadaiwa kutumia kushambulia Israeli kupitia kivuko cha mpaka cha Erez mnamo Oktoba 7. Jeshi la Israel limesema mnamo Desemba 17, 2023 kwamba limegundua handaki kubwa zaidi la Hamas katika Ukanda wa Gaza hadi sasa, mita mia chache tu kutoka kwenye kivuko cha mpaka cha Erez. © Jack Guez / AFP
Matangazo ya kibiashara

"Mtandao huu mkubwa wa handaki, ambao umegawanywa katika matawi kadhaa, unaenea kwa zaidi ya kilomita nne na unakuja mita 400 tu kutoka kivuko cha Erez" kati ya Israeli na Ukanda wa kaskazini wa Gaza, jeshi la Israeli limesema katika taarifa. Handaki hiyo ina mfumo wa bomba, umeme, uingizaji hewa, mifereji ya maji taka, mitandao ya mawasiliano na reli. Ardhi yake imetengenezwa kwa udongo uliopigwa na kuta zake zimetengenezwa kwa saruji iliyoimarishwa, isipokuwa kwenye kituo chake, kilichoimarishwa na silinda ya chuma takriban sentimita moja na nusu kwa kipenyo.

Wakati huo huo Malori 79 ya misaada ya kibinadamu yamepita Jumapili hii kupitia kituo cha mpaka cha Kerem Shalom, kilichofunguliwa leo.

Ili kupunguza uhaba wa chakula, maji, dawa na mafuta, tangu kuanza kwa vita na kuzingirwa kwa jumla kwa Ukanda wa Gaza ulioanzishwa mnamo Oktoba 9, Israeli ilianza kutoa msaada wa kibinadamu kutoka kivuko cha Kerem Shalom, kwenye mpaka na Misri.

Chanzo kutoka Shirika la Hilali Nyekundu la Misri, sawa na Msalaba Mwekundu, kimethibitisha kuwa lori 79 zilipitia kituo hiki siku ya Jumapili.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.