Pata taarifa kuu
IRAN-MAREKANI-EU

Iran yashtumiwa kwa kuanza kurutubisha madini ua Uranium

Marekani  na mataifa ya Ulaya yamelaani hatua ya Iran kuanza tena urutubishaji wa madini ya Uranium kwa asilimia 20 kinyume na makubaliano ya Kimataifa yaliyokubaliwa mwaka 2015.

Kituo cha Bushehr, kinachotumiwa na Iran kwa mradi wake wa Nyuklia
Kituo cha Bushehr, kinachotumiwa na Iran kwa mradi wake wa Nyuklia ATTA KENARE AFP/File
Matangazo ya kibiashara

Kituo cha Kimataifa kinachoshughulia nishati ya Atomic, kinaonya kuwa  hatua hiyo ya Iran  inahatarisha mazungumzo ambayo yamekuwa yakiendelea kujaribu kupata suluhu ya suala hilo.

Ned Price, msemaji wa Wizara ya Mambo ya nje wa Marekani, amesema uongozi wa rais Joe Biden unasikitishwa na mwenendo wa Iran.

Inazua wasiwasi kuwa Iran inachagua kutosimamia utekelezwaji wa mkataba uliokubaliwa  kwa majarbio inayofanya, hakika hii inasikitisha sana, tunapenda kutoa wito kwa Iran kuacha kurudi nyuma na kurejea kwenye mazungumzo huko Vienna ili kumalizia kazi iliyoanza mwezi Aprili, mazungumzo ambayo yamefikia  hatua ya sita.

Mataifa ya Magharibi yanahofia kuwa, iwapo Iran itafanikiwa katika mpango wake, itakuwa inakaribia kutengeneza  silaha za nyuklia na hivyo kutishia usalama wa dunia.

Tangu rais wa zamani  wa Marekani Donald Trump aiondoe nchi yake kwenye mpango wa pamoja wa makubaliano kuhusu mradi huu (JCPOA) mwaka 2018, Iran imeendelea kwenda kinyume na makubaliano ya kusitisha urutubishaji wa uranium.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.