Pata taarifa kuu
AFGHANISTAN-USALAMA

Askari 30 wa Afghanistan wauawa na Taliban

Askari thelathini wa Afghanistan wameuawa Jumatano wiki hii katika shambulio la kuvizia la Taliban katika jimbo la Magharibi la Badghis, gavana wa jimbo hilo amesema.

Majeshi ya Afghanistan yaendelea kupambana dhidi ya wapiganaji wa Taliban katika maeneo mbali ya nchi hiyo.
Majeshi ya Afghanistan yaendelea kupambana dhidi ya wapiganaji wa Taliban katika maeneo mbali ya nchi hiyo. REUTERS/Mohammad Ismail
Matangazo ya kibiashara

Hili ni shambulio la kwanza kubwa la Taliban lililogharimu maisha ya askari wengi wa Afghanistan tangu kutangazwa kusitishwa mapigano kwa muda wa siku tatu, siku ya Jumapili, kutokana na sherehe za Eid el Fitr.

Majeshi ya Serikali pia yasitisha mapigano. Muda huo ungelimalizika leo Jumatano, lakini serikali ya Afghanistan ilikua iliongeza siku kumi.

Wapiganaji wa Taliban waliruhusiwa kushiriki mwishoni mwa wiki iliyopita katika sherehe za kumaliza mwezi mtukufu wa Ramadhan katika miji kadhaa ya Afghanistan.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.