Pata taarifa kuu
MAREKANI-ISRAEL-PALESTINA-USALAMA

Wapalestina 45 wauawa katika makabiliano na jeshi la Israeli

Waandamanaji arobaini na watano, raia wa Palestina, wameuawa katika mapigano na vikosi vya Israeli kwenye mpaka kati ya Ukanda wa Gaza na Israeli, mwandishi wa RFI ameripoti.

Maandamano yenye vurugu yasababisha vifo vya watu 37 kwenye mpaka kati ya Gaza na Israel.
Maandamano yenye vurugu yasababisha vifo vya watu 37 kwenye mpaka kati ya Gaza na Israel. REUTERS/Ibraheem Abu Mustafa
Matangazo ya kibiashara

Watu 900 wamejeruhiwa, ikiwa ni pamoja na 450 ambao wamepigwa risasi.

Hii ni idadi kubwa ya vifo kutokea kwenye mpaka wa Israel tangu kuanza kwa "Mandamano makubwa" ya Wapalestina manamo Machi 30 .

Maandamano haya yanatazamiwa kuendelea Jumanne, Mei 15, siku ambayo Wapalestina wanaita "Nakba" ( "janga"), ikimaanisha kufukuzwa kwa mamia ya maelfu ya Wapalestina wakati taifa la Israel lilipoundwa mnamo mwaka 1948.

Tangu mwishoni mwa mwezi Machi, waandamanaji 82 waliuawa na vikosi vya usalama vya Israel kwenye mpaka wa Gaza. Wakati huo hakuna raia wa Israel aliyeuawa.

Jeshi la Israel lilirusha vipeperushi katika Ukanda wa Gaza, na kuwataka wakazi wa eneo hilo "kutotumiwa" na kundi la Hamas, ambalo lina mamlaka katika Ukanda wa Gaza kwa zaidi ya miaka kumi, pia kuwataka kutothubutu kukaribia mpaka wa Israel na ukanda huo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.