Pata taarifa kuu
MAREKANI-SYRIA

Marekani yasema Syria inapanga kutumia silaha za kemikali kuwashambulia raia

Marekani inasema serikali ya Syria inafanya maandalizi ya kuwashambulia raia wa kawaida kwa kutumia silaha zake za kemikali.

Shambullizi la awali la silaha za kemikali mjini Homs nchini Syria
Shambullizi la awali la silaha za kemikali mjini Homs nchini Syria REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Ikulu ya Marekani imesema uchunguzi wake umeonesha wazi kuwa maandalizi yanafanyika kutekeleza shambulizi hilo kama ilivyokuwa mwezi Aprili mwaka huu na kusababisha maafa makubwa ya watu.

Wsshington DC sasa inaonya kuwa itaichukulia hatua kali  serikali ya rais Bashar Al Assad ikiwa itatekeleza shambulizi hilo.

Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Nikki Haley amesema Urusi na Iran pia watawajibikia shambulizi hilo litatokea.

“Shambulizi lolote kwa raia wa Syria, tutailaumu serikali ya Urusi na Iran ambayo inamuunga mkono rais Bashar Al Assa",  amesema Nikki.

Serikali ya Damascus hata hivyo imekuwa ikikanusba madai yoyote ya kutumia silaha zake za nyuklia kuwashambulia raia wa nchi hiyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.