Wimbi la Siasa
Usalama nchini Uganda na ukanda baada ya mashambulio ya ADF
Imechapishwa:
Cheza - 10:04
Kundi la waasi la ADF Lenye asili nchini Uganda ila limekuwa likitikileza mashambulio mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ,limewauwa watu 42 nchini Uganda baada ya kushambulia shule ya sekondari eneo la Kasese
Matangazo ya kibiashara
ADF linaonekana kuwa tishio baada ya ripoti ya umoja wa mataifa kuonesha ADF imekuwa ikifadhiliwa na kundi la Kijihadi la Islamic State tangu mwaka 2019. Kuna hofu mtandao wake ADF unaweza kusambaaa zaidi baada ya ripoti hiyo kusema Islamic State imekuwa ikiwatumia watu kutoka mataifa ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini.