Mapambano kupunguza matumizi ya Tumbaku na mchango wa sekta binafsi katika afya
Imechapishwa:
Cheza - 10:07
Mataifa ya ulimwengu yanapoadhimisha siku ya Tumbaku Mei 31,kuna hofu juhudi za kupunguza matumizi ya tumbaku zinaonekana kurudishwa nyuma na ukiukaji wa sheria za kupambana na matumizi ya tumbaku
Sheria kuhusu ushuru unaotozwa kwenye bidhaa za tumbaku bado haifuatwi kikamilifu .Wafanyibiashara wanaouza sigara chini ya pakiti moja wanatuhumiwa vile vile kurudisha mapambano ya kupunguza matumizi ya tumbaku.Isitoshe kampuni zinazotengeneza bidhaa hizo zimekuja na bidhaa mpya ambazo zinawavutia watumizi wa umri mdogo na pia wanawake .
Aidha kwenye makala haya tunakufahamisha kuhusu juhudi za sekta binafsi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kuchangia kupunguza idadi ya raia wanaoumwa kwa kuwatuza na kuwasaidia kuepukana na magonjwa haswa yasiyoambukizwa.