Shirika la afya duniani limeonya kuhusu kuongezeka kwa watu walio na uzito wa kupitiliza ,hali inayowaweka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa
Shirikisho lilaloangazia unene ulimwenguni ,limesema zaidi ya nusu ya watu ulimwengu watakuwa na uzito wa juu au unene wa kupitiliza kufikia mwaka 2035 ikiwa hatua madhubuti kudhibiti hali hiyo hazitachukuliwa
Mataifa yanayoendelea na maskini barani Afrika na Asia yanatazamiwa kushuhidia hali hii.
Baadhi ya sababu zinazochangia hali hii ni ulaji na watu kushindwa kufanya mazoezi.Katika makala haya tunazungumza na watu wanaopambana kupunguza uzito,watalaam wa afya na pia wapishi kuelewa nini kinaweza kusaidia mtu kufanya chaguo zuri kuhusu chakula na mifumo ya maisha inayofanya mtu kuishi maisha yenye afya.