China yakamilisha siku tatu za Mazoezi yanayolenga kuivamia Taiwan
Imechapishwa:
Cheza - 09:56
China imefanya mazoezi ya siku tatu ya kijeshi huku ikikisiwa kuwa na mpango wa kulenga maeneo muhimu ya Taiwan.Wakati jeshi la China likifanya mazoezi hayo kuzunguka kisiwa hicho, Marekani iliitaka China kuonyesha kujizuia.
Mwishoni mwa juma maafisa wa ulinzi mjini Taipei waliishutumu Beijing kwa kutumia ziara ya Rais Tsai wa Marekani kama kisingizio cha kufanya mazoezi ya kijeshi, ambayo yamevuruga pakubwa amani, utulivu na usalama katika eneo hilo.
Kufuatia swala hili tumewauliuza wasikilizaji iwapo wanadhani hii itaongeza mvutano kati ya Marekani na China? na Je, wanaamini kuwa China inaweza kuivamia Taiwan ? na haya yalikua maoni yao.