Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, anafanya ziara kwa mataifa manne ya Africa, ikiwemo Jumhuri ya Kidemokrasia ya Congo, katika hatua kujaribu kuimarisha uhusiano kati ya Ufaransa na mataifa ya Africa .
Ziara yake inajiri wakati huu wanajeshi wa taifa lake wakiwa wametimuliwa katika mataifa ya Mali na Burkina Faso, mataifa hayo yakitumu Ufaransa kwa uchangia utovu wa usalama katika mataifa hayo.
Hata hivyo katika hotuba yake kwa taifa siku ya jumatatu juma hili, rais Macron alitetea taifa lake dhidi ya mataifa ya kuchochea ukosefu wa usalama eneo la sahel, akituhumu mataifa hayo kwa kushindwa kupambana na ugaidi.
Tumekuuliza je ziara ya rais Macron ina manufaa yoyote kwa mataifa ya Africa
Haya hapa baadhi ya maoni yako.