Pata taarifa kuu
UGANDA

Uganda yamshikilia mwanaharakati kwa kumkosoa mke wa raisi Museven

Uganda inamshikilia mwanaharakati na muhadhiri wa chuo kikuu cha Makerere kwa kumkosoa mke wa raisi wa Uganda kupitia mtandao wa kijamii.

Janet Museven Waziri wa Elimu wa Uganda na mke wa raisi Yoweri Museven
Janet Museven Waziri wa Elimu wa Uganda na mke wa raisi Yoweri Museven
Matangazo ya kibiashara

Stella Nyanzi alimkosoa Bi Janet Museveni, ambaye ni waziri wa elimu kupitia ukurasa wake wa face book baada ya serikali kusema inaandaa mpango wa kugawa taulo za kike kwa wasichana wanafunzi ambao wapo katika mazingira magumu ya kupata vifaa hivyo.

Msemaji wa polisi Emilian Kayima amethibitisha kukamatwa kwa Stela Nyanzi ambaye atafikishwa mahakamani siku ya jumatatu jijini kampala kwa matumizi mabaya ya mtandao na kuvunja sheria ya mawasiliano ya mwaka 2011.

Kwa mujibu wa Kayima Bi Stella Nyanzi amekuwa akichapisha masuala yanayotazamwa kama vita kupitia mtandao wa kijamii ambayo hayana maslahi kwa taifa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.