Pata taarifa kuu

Wanajeshi wa Afrika Kusini wauuawa mashariki mwa DRC

Nairobi – Wanajeshi wawili wa Afrika Kusini wameuawa wakati wengine watatu wakiripotiwa kujeruhiwa katika shambulio kwenye moja ya kambi zao za kijeshi nchini DRC ambapo walitumwa kukabiliana na makundi ya waasi.

Mapigano ya hivi majuzi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yamesababisha makumi ya maelfu ya watu kuyahama makazi yao
Mapigano ya hivi majuzi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yamesababisha makumi ya maelfu ya watu kuyahama makazi yao © ALEXIS HUGUET / AFP
Matangazo ya kibiashara

Maofisa hao wamekuwa waathiriwa wa kwanza tangu Afrika Kusini kuanza kuwatuma maofisa wake wa jeshi nchini DR Congo mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka uliopita.

Shambulio hilo limetokea katika mji wa Sake, karibia kilomita 27 Magharibi mwa mji wa Goma.

Kwa mujibu wa taarifa iliochapishwa kwenye ukurasa wa X, jeshi la Afrika Kusini limesema uchunguzi umeanza kuhusiana na tukio hilo.

Wanajeshi wa Afrika Kusini pamoja na wanajeshi kutoka Tanzania na Malawi ni sehemu ya ujumbe wa Kusini mwa Afrika ulio nchini DR Congo (SAMIDRC), ambao ulitumwa kusaidia serikali kuleta amani, usalama na utulivu mashariki mwa nchi hiyo kunakokabiliwa machafuko.

Jumatatu iliyopita, rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa aliamuru kutumwa kwa wanajeshi 2,900 nchini DRC.

Mapigano ya hivi majuzi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yamesababisha makumi ya maelfu ya watu kuyahama makazi yao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.