Pata taarifa kuu

DRC: Tanzania yatetea hatua ya kushiriki kwenye kikosi cha SADC

Nairobi – Tanzania imetetea hatua ya kushiriki kwenye kikosi cha kijeshi kutoka nchi za Jumuiya ya Kusini mwa Afrika SADC, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ikisema inaunga mkono jitihada za kikanda chini ya mikataba ya Nairobi na Luanda ili kurejesha usalama katika eneo hilo.

Tanzania imetetea hatua ya kushiriki kwenye kikosi cha kijeshi kutoka nchi za Jumuiya ya Kusini mwa Afrika SADC
Tanzania imetetea hatua ya kushiriki kwenye kikosi cha kijeshi kutoka nchi za Jumuiya ya Kusini mwa Afrika SADC © SADC
Matangazo ya kibiashara

Waziri wa Mambo ya nje, January Makamba, ametoa ufafanuzi huo, baada ya madai kuwa wanajeshi wake wameendelea kurusha mabomu kuwalenga raia, katika operesheni ya kupambana na waasi wa M 23.

Makamba amesisitiza kuwa Tanzania, haishiriki kwenye operesheni hiyo peke yake bali, ipo kwenye kikosi cha SADC na inaunga mkono mikataba ya kikanda kurejesha amani jimboni Kivu Kaskazini.

Mapigano yamekuwa yakiripotiwa kati ya waasi wa M23 na wanajeshi wa serikali
Mapigano yamekuwa yakiripotiwa kati ya waasi wa M23 na wanajeshi wa serikali © ALEXIS HUGUET / AFP

Siku chache zilizopita, kundi la M23 lilitoa taarifa kulalamikia jeshi la Tanzania kuwalenga raia, kwenye maeneo wanayodhibiti na kuapa kujilinda.

Wakati hayo yakijiri, wiki hii kumeshuhudiwa mapigano makali kati ya jeshi la DRC na waasi wa M 23, huku kukiwa na ripoti kuwa waasi hao walikuwa mjini Sake, umbali wa Kilomita 25 kutoka mjini mkuu wa Kivu Kaskazini Goma.

Waziri wa ulinzi wa DRC Jean-Pierre Bemba
Waziri wa ulinzi wa DRC Jean-Pierre Bemba AFP - ARSENE MPIANA

Waziri wa Ulinzi,Jean Pierre Bemba, jana alitembelea  Goma, na kuwahakikishia wakaazi wa mji huo serikali jijini Kinshasa itahakikisha kuwa wanalindwa dhidi ya hatari yoyote kutoka kwa waasi wa M 23.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.