Uganda: Walinda usalama wamezingira afisi za upinzani
Nairobi – Maofisa wa polisi nchini Uganda na wenzao wa jeshi, wameripotiwa kuweka vizuizi katika afisi kuu za chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP), kinachoongozwa na mwanasiasa wa upinzani Bobi Wine.
Imechapishwa:
Katika taarifa yake kwenye mtandao wa X, chama hicho kimethibitisha kuzuiliwa kwa afisi zake katiak eneo la Kamwokya.
There is heavy military deployment at our secretariat in Kamwokya, and they are currently off limits. This comes after we announced that we would be holding a special prayer session for our comrades who have fallen victims of the regime’s brutal actions. What a shame. pic.twitter.com/vMmbkSleCa
— National Unity Platform (@NUP_Ug) October 9, 2023
Kwa mujibu wa kiongozi wa chama hicho, Bobi Wine, maofisa wa serikali wamevamia makao makuu ya chama chake na kwamba wamewazuia watu kuingia au kutoka kwenye majengo ya chama hicho.
Mwanamuziki huyo wa zamani ambaye kwa sasa ni mwanasiasa aliandika kwenye mitandao wake wa kwamba hatua hiyo ya maofisa wa usalama inalenga kuzuia hafla ya maombi ambayo NUP ilikuwa imepanga kufanya katika ofisi yake Kampala siku ya Jumatatu.
Update: Police block entry to NUP party headquarters in Kamwokya ahead of their planned press briefing. #NTVNews
— NTV UGANDA (@ntvuganda) October 9, 2023
More Details to follow. pic.twitter.com/IdKxeVKWPQ
Wiki iliyopita, polisi walimsindikiza Bobi Wine hadi nyumbani kwake baada ya kurejea Uganda kutoka Afrika Kusini, wakisema kuwa hatua hiyo ilikuwa ni kumzuia kuandaa maandamano.
Pia waliwazuilia makumi ya wafuasi wa Bobi Wine kwa madai kwamba walichochea vurugu na kupanga maandamano ambayo hayakuwa na kibali.
Bobi Wine amewakosoa maafisa hao wa usalama kwa hatua hiyo.