Pata taarifa kuu

Kenya na Indonesia kuimarisha ushirikiano

Nairobi – Kenya na inalenga kuimarisha uhusiano wake na nchi ya Indonesia ilikuinua viwango vya kibiashara kati ya mataifa hayo mawili.

Marais wa Kenya na Indonesia wameahidi kuimarisha ushirikiano
Marais wa Kenya na Indonesia wameahidi kuimarisha ushirikiano © Statehouse Kenya
Matangazo ya kibiashara

Katika kikao kati ya rais wa Kenya William Ruto na mgeni wake rais wa Joko Widodo, rais Ruto mataifa hayo mawili pia yalenga kujiendeleza katika sekta ya uwekezaji.

Uwekezaji kati ya nchi hizo mbili katika kipindi cha mwaka uliopita, ulikadiriwa kuzalisha zaidi ya dolla milioni mia sita.

Mataifa hayo pia yametia saini mikataba ya ushirikiano
Mataifa hayo pia yametia saini mikataba ya ushirikiano © Statehouse Kenya

Kwa mujibu wa hotuba ya rais Ruto, nchi hizo aidha zinatoa kipau mbele katika sekta za nishati, madini na uzalishaji wa mafuta.

Kenya pia inalenga kupata uungwaji mkono kutoka kwa nchi ya Indonesia kuisaidia kuingia katika masoko ya nchi za kusini mashariki mwa nchi za Asia, eneo ambalo uchumi wake unakuwa kwa kasi katika ukanda wa bara Asia.

Nchi hizo zinalenga kuimarisha ushirikiano katika sekta za madini na nishati
Nchi hizo zinalenga kuimarisha ushirikiano katika sekta za madini na nishati © Statehouse Kenya

Kwa upande wake rais Widodo amesema nchi yake itafanya kazi na Kenya kuendeleza ukuwaji wa mataifa hayo mawili.

Kiongozi huyo pia amesisitiza kuwa nchi yake inalenga kuhakikisha kwamba ushirikiano kati yake na Kenya unaleta faida kwa raia wa nchi husika.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.