Rais Museveni ameituhumu benki kuu ya dunia kwa kutumia vitisho dhidi ya serikali yake
Rais wa Uganda Yoweri Museveni, ameithumu benki kuu ya dunia kwa kujaribu kutumia vitisho dhidi ya serikali yake kutokana na sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.
Imechapishwa:
Tamko la rais Museveni linakuja baada ya tangazo la benki kuu ya dunia kwamba ilikuwa inasitisha mikopo yoyote mpya kwa nchi hiyo kwa misingi kwamba sheria dhidi ya mahusiano ya jinsia moja inakinzana na maadili yake.
Katika taarifa iliyotumwa kwenye mitandao ya kijamii, Rais Museveni alisema kuwa Uganda itajiendeleza kwa mkopo au bila.
Ugandans, especially the Bazzukulu.
— Yoweri K Museveni (@KagutaMuseveni) August 9, 2023
Greetings. Things are moving well in Uganda in spite of the corruption of some Public Servants and some elements of the political class.
Last night, an official from the World Bank rang me to alert me about the statement from that Bank… pic.twitter.com/vCJMUcD7CZ
Kwa mujibu wa rais Museveni, ni bahati mbaya kwamba benki ya dunia ilikuwa inawalazimisha kuacha imani, utamaduni, kanuni na uhuru wao, kwa kutumia pesa.
"Kwa kweli wanadharau Waafrika wote. Hatuhitaji shinikizo kutoka kwa mtu yeyote kujua jinsi ya kutatua matatizo katika jamii yetu. Ni matatizo yetu,” aliongeza.
Rais Museveni alitia saini sheria dhidi ya ushoga mwezi Mei, ambayo inatoa hukumu ya kifo kwa ushoga uliokithiri na kifungo cha miaka 20 jela kwa kuendeleza ushoga.
Sheria hiyo imepingwa na mashirika ya haki za binadamu nchini Uganda na kimataifa. Umoja wa Mataifa, Marekani na mataifa mengine pia yamelaani sheria hiyo mpya.
Benki ya dunia inaungana na Marekani katika kuweka vikwazo dhidi ya Uganda kutokana na sheria ya Kupinga Ushoga.