Pata taarifa kuu

Kenya: Serikali kuwakabili wapiganaji wa Al-Shabaab

Nairobi – Waziri wa ulinzi nchini Kenya Adan Duale amekiiri kuwakabili kwa nguvu wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab kwenye maeneo ya mpaka wa taifa hilo la Afrika Mashariki na nchi jirani ya Somalia.

Al-Shabaab, wamekuwa wakitekeleza mashambulio katika maeneo jirani na Somalia katika upande wa Kenya
Al-Shabaab, wamekuwa wakitekeleza mashambulio katika maeneo jirani na Somalia katika upande wa Kenya AFP/Archivos
Matangazo ya kibiashara

Kauli ya waziri Duale inakuja wakati huu kasi ya mashambulio yanayotekelezwa na wapiganaji hao kwenye miji inayopakana na Somalia ikionekana kuongezeka katika siku za hivi majuzi.

Duale aidha amewaonya amesema atafanya kazi kwa ukaribu na waziri wa usalama wa ndani Kithure Kindiki kuwanasa Wakenya wanaoshirikiana na Al-Shabaab nchini humo.

Waziri huyo ametembelea miji mitano kwenye mpaka wa Kenya-Somalia, miji ambazo zimekuwa zinakabiliwa na changamoto za kiusalama kutoka kwa kundi hilo kaskazini mashariki ya Kenya.

Viongozi kwenye maeneo hayo wametoa wito kwa jamii kushirikiana na walinda usalama katika mapambano dhidi ya Al-Shabaab.

Onyo la serikali ya Kenya linakuja baada ya watu wanaodhaniwa kuwa wapiganaji wa Al- Shabaab kutekeleza mashambulio kwenye maeneo matatu tofauti katika kaunti ya Mandera kaskazini Mashariki ya Kenya siku ya Ijumaa asubuhi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.