Pata taarifa kuu

DRC: Mjumbe wa Papa Francis amezuru Goma

NAIROBI – Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,  Luis Antonio Tagle  mjumbe maalum wa kiogozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis, ametembelea Goma, eneo linalokabiliwa na utovu wa usalama kutokana na mashabulizi ya mara kwa mara yanayotekelezwa na makundi ya waasi, na kuendesha misa maalum iliyoshirikisha madhebu mbalimbali, kuombea amani.

Kadinali Luis Antonio Tagle, amezuru Goma
Kadinali Luis Antonio Tagle, amezuru Goma AP - Andrew Medichini
Matangazo ya kibiashara

Kwa shangwe na furaha, maelfu ya raia  jijini GOMA wameishiriki Ibada hiyo iliyoongozwa na  Luis Antonio Tagle , mjumbe wa Papa FRANCIS ,ambaye ametoa wito wa kuwepo kwa amani, ushirikiano pamoja na kutoa wito wa kuwepo usalama mashairki ya DRC.

Hapa Goma tuwe pamoja , tumwe chumvi ya dunia na nuru ya ulimwengu , tunatoa wito wa kuwepo kwa msamaha na upatanisho na amani ya kudumu.” alisema   Luis Antonio Tagle.

00:14

LUIS ANTONIO TAGLE

Baadhi ya raia wa Mji wa Goma wakristo na wasiokuwa wa Kristo walioshiriki Ibaada hiyo walizungumza na mwandishi wetu wa Goma baada ya ibaada.

Tunamshukuru kiongozi huyo kwa kutembelea  ila tunacho omba kutoka kwake  ni kuzidi sana kutuombea tupate amani jimboni mwetu Kivu kaskazini.” alisema mmoja wa waliohudhuria ibaada.

00:12

Mkaazi wa Goma

Baada ya misa hiyo iliyowakusanya wakristo kutoka madhebu mbalimbali lakini pia viongozi wa Serikali na Mashirika ya kiraia , Luis Antonio Tagle anatarajiwa kuzuru kambi ya KANYARUCHINYA wilayani nyiragongo ambapo atakutana na watu waliokimbia makazi yao kutokana na mashambulio ya watu wenye silaha.

CHUBE NGOROMBI GOMA RFI KISWAHILI

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.