Pata taarifa kuu

Uganda: Rais Museveni azungumza wakati huu kukiwepo na uvumi kwamba amefariki

NAIROBI – Rais wa Uganda Yoweri Museveni kupitia ukurasa wake wa twitter Jumapili usiku ameandika kuwa bado anaendelea na kujitenga baada ya kuambukizwa uviko 19.

 Rais wa Uganda Yoweri Museveni, kupitia ukurasa wake wa twitter amesema anaendelea kujitenga baada ya kuambukizwa uviko 19
Rais wa Uganda Yoweri Museveni, kupitia ukurasa wake wa twitter amesema anaendelea kujitenga baada ya kuambukizwa uviko 19 REUTERS - ABUBAKER LUBOWA
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii ya rais Museveni, inakuja wakati huu taarifa kwenye mitandao ya kijamii ikidai kuwa kiongozi huyo wa Afrika Mashariki amefariki baada ya kuambukizwa virusi hivyo.

Museveni aliambukiza uviko 19 tarehe saba ya mwezi Juni kabla ya rais huyo kutangaza siku moja baadae kwamba anachukua likizo kutoka kazini.

"Habari.  Ni siku tano sasa tangu niambukizwe. Usiku uliopita nilala vyema nikaamka saa kumi.” kiongozi huyo alichapisha kwenye ukurasa wake wa twitter.

Ametoa wito kwa raia wa Uganda kuwenda kupokea chanjo ya uviko 19 na wazee kwenda kuchomwa nyongeza ya chanjo.

Madai yameibuka kwenye mtandao wa twitter katika kipindi cha siku chache zilizopita kwamba rais Museveni alikuwa amepelekwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi kabla ya kufariki kutokana na makali ya maambukizi ya corona.

Mwezi uliopita, shirika la afya duniani WHO mwezi jana lilitangaza kwamba maambukizi ya uviko 19 kwa sasa sio janaga la kitaifa japokuwa WHO ilionya kwamba virusi hivyo vitandelea kubadilika.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.