Pata taarifa kuu
HAKI

ICC: Kesi dhidi ya mfanyabiashara Félicien Kabuga kuanza Septemba 29 Hague

Kesi dhidi ya mfanyabiashara na mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Félicien Kabuga, sasa itaanza tarehe 29 mwezi Septemba kwenye Mahakama ya Kimataifa ya ICC jijini Hague. 

Felicien Kabuga, mmoja wa washukiwa wakuu wa mwisho katika mauaji ya kimbari ya Rwanda mwaka 1994, kwenye bango lililotundikwa katika ofisi ya kitengo cha ufuatiliaji wa watu waliohusika katika mauaji ya halaiki mjini Kigali.
Felicien Kabuga, mmoja wa washukiwa wakuu wa mwisho katika mauaji ya kimbari ya Rwanda mwaka 1994, kwenye bango lililotundikwa katika ofisi ya kitengo cha ufuatiliaji wa watu waliohusika katika mauaji ya halaiki mjini Kigali. AFP
Matangazo ya kibiashara

Uamuzi huo, umefikiwa na Majaji wa Mahakama hiyo, baada ya Kabuga mwenye umri wa miaka 87 kufika mbele yao kusikiliza utaratibu wa namna kesi yake itakavyoendeshwa. 

Kabuga,alikamatwa na kuzuiwa nchini Ufaransa mwaka uliopita, baada ya kukwepa kukamatwa kwa zaidi ya miaka 20. Aidha, Majaji wameamua kuwa, kwa sababu ya hali yake ya kiafya ataruhusiwa kuhudhuria vikao hivyo kwa njia ya vídeo kama italazimika kufanya hivyo. 

Wakati akiwa nchini Rwanda, alikuwa rais wa kituo cha redio na Televisheni Libre des Mille Collines, ambazo zilitumiwa kutangaza kuuawa kwa Watutsi wakati wa mauaji ya kimbari mwaka 1994. 

Anatuhumiwa kuhusika kupanga mauaji ya kimbari, uchochezi yaliyosababisha mauaji hayo na uhalifu dhidi ya binadamu. 

Mauaji ya kimbari nchini Rwanda, yalisababisha vifo vya watu 800,000, wengi wakiwa Watutsi. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.