Watu wengi wauawa katika shambulio la kujitoa mhanga Kabul
Watu wengi wameuawa mapema Jumanne hii asubuhi mjini Kabul katika shambulio la kujitoa mhanga lililotekelezwa na wapiganai wa kundi la Taliban dhidi ya majengo ya serikali yalio karibu na makao makuu ya Idara ya Ujasusi nchi Afghanistan.
Imechapishwa:
Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani anasema kuwa watu wengi wameuawa ana wengine kujeruhiwa kufuatia shambulizi la kujitoa mhanga wakati wa shughuli nyingi kwenye mji mkuu wa Afghanistan Kabul.
"Rais analaani kwa kauli kali shambulio la kigaidi la asubuhi hii ambalo limesababisha vifo vya watu wengi na watu wengi waliojeruhiwa miongoni mwa raia wenzutu," kwa ujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya rais.
Kundi la wapiganaji wa Taliban limetangaza kuendesha shambulio hilo. Hivi karibuni kundi la wapiganaji wa Taliban lilitangaza kuwa mbioni kuanzisha mashambulizi katika nchi nzima ya Afghanistan.