Pata taarifa kuu
Mo Ibrahim - Tuzo

Tuzo ya amani ya Mo Ibrahim imekosa mshindi kwa mara nyingine tena

Tuzo la Mo Ibrahim, ambalo hutolewa kwa viongozi wastaafu waliohudumu kwa kuheshimu sheria na utawala bora, imekosa mshindi kwa mwaka wa nne sasa tangu kuundwa kwake miaka saba iliopita.

Mo Ibrahim
Mo Ibrahim
Matangazo ya kibiashara

Katika mkutano na waandishi wa habari  mjini London, wakfu wa Mo Ibrahim umesema kuwa baada ya kutafakari kwa makini, wamemkosa mshindi wa tuzo hiyo mwaka huu wa 2013.

tuzo hiyo ya Mo Ibrahim hutolewa kwa kiongozi aliye teuliwa katika misingi ya kidemokrasia na amabye amestaafu kwa kipindi cha miaka mitatu, na ambaye uongozi wake  uliheshimu sheria na misingi ya utawala bora.

Tuzo hiyo ilianzishwa na mfanyabiashara bilionea raia wa Uingerwza mwenye asili ya Sudan, Mo Ibrahim hutoa dola milioni 5 kwa kipindi cha miaka kumi na dola laki mbili kila mwaka hadi kiongozi huyo atakapofariki.

Mbali na kitita hicho dola laki mbili hutolewa kwa mradi wowote unaoungwa mkono na mshindi wa tuzo hiyo kwa kipindi cha miaka kumi.

Huu umekuwa ni mwaka wa nne tuzo hiyo inakosa mshindi tangu kuanzishwa kwake miaka 7 iliopita. Mtu wa kwanza kupewa tuzo hiyo alikuwa ni Joachim Chisano rais mstaafu wa Msumbiji, mwaka 1995, Festus Mogae wa Botswana 2008 pamoja na
Pedro Pires wa Cape Verde mwaka 2011.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.