Pata taarifa kuu
HAITI-URUGUAY

Kijana aliyefanyiwa vitendo vya udhalilishaji na askari wa Uruguay nchini Haiti aanza kutoa ushahidi wake

Kijana mwenye umri wa miaka 19 rais wa Haiti anayedaiwa kufanyiwa vitendo vya udhalilisha na askari wa Uruguay waliokuwa wakilinda amani nchini humo chini ya mwavuli wa Umoja wa Mataifa hii leo amepanda kizimbani kutoa ushahidi wake.

Matangazo ya kibiashara

Kijana huyo na familia yake waliwasili nchini Uruguay hapo jana tayari kuanza kusikilizwa kwa kesi yake dhidi ya wanajeshi nane wa nchi hiyo waliokuwa nchini Haiti kulinda amani na kudaiwa kumdhalilisha kijana huyo.

Kijana huyo alifikishwa mbele ya jaji wa mahakama kuu ya Uruguay kwenye kesi ambayo inasikilizwa kwa usiri mkubwa ikiwa ni ushahidi wake wa mwanzo kuwasilisha kwenye mahakama kuhusu askari hao.

Kijana huyo ambaye anadaiwa kufanyiwa vitendo vya udahlilishaji na wanajeshi hao mwezi wa tisa mwaka jana, picha za video zilizopigwa na mmoja wa wanajeshi hao zilisambaa kwenye mtandao na kuchafua jeshi la Uruguay.

Mkanda wa video uliowaonesha wanajeshi hao wakimfanyia vitendo vya udhalilishaji kijana huyo, iliamsha hisia za wananchi wa Haiti ambao waliamua kuingia mtaani kushunikiza kuondolewa kwa vikosi vyote vya Umoja wa Mataifa nchini humo.

Jaji aliyeteuliwa kusikiliza kesi hiyo mara baada ya kusikiliza ushahidi wa kijana huyo ataamua endapo wanajeshi hao wanakesi ya kujibu au la.

Vyombo vya habari nchini humo vimedai kuwa

Uruguayan media reports said the Haitian man would be asked to identify his alleged attackers.

The marines are also being questioned by the judge.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.