Marekani yaanzisha utekelezaji wa vikwazo kwa wanunuzi wa mafuta Iran
Fukuto la mgogoro wa Iran limeendelea ambapo raisi wa marekani Barack Obama amethibitisha kuanzishwa kwa vikwazo mahususi kwa washirika na wanunuzi wa mafuta yanayopatikana nchini Iran.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Katika taarifa yake raisi Obama alisema washirika wa marekani wakigomea mafuta ya Iran hawatadhurika kwakuwa kuna mafuta ya kutosha katika soko la dunia.
Mpango huo utaiwezesha Marekani kuchukua hatua dhidi ya benki za kigeni ambazo bado zinajihusisha na mfauta ya Iran.
Iran inakabiliwa na shinikizo la kimataifa juu ya wasiwasi wa nchi hiyo kujitajirisha kupitia mpango wake wa uzalishaji wa nyuklia jambo ambalo mataifa ya magharibi yanaituhumu Iran kuzalisha silaha za nyuklia.