Pata taarifa kuu
UFARANSA, UINGEREZA

Ufaransa na Uingereza zasaini mkataba kuhusu nyuklia, zainyoshea kidole Syria

Ufaransa na Uingereza zimesaini mkataba wa kuendeleza ushirikiano katika masuala ya nishati ya nyuklia kwa ajili ya matumizi ya kawaida hatua ambayo inatarajiwa kusukuma maendeleo katika nchi hizo.Pamoja na kusukuma maendeleo mpango huo utasaidia kuongeza fursa zaidi za biashara zenye thamani ya Euro milioni 500 baina ya pande hizo mbili. 

Kulia na Rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy na akishikana mkono na Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron leo wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari
Kulia na Rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy na akishikana mkono na Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron leo wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari REUTERS/Benoit Tessier
Matangazo ya kibiashara

Aidha mpango huo wa Ufaransa na Uingereza utaongeza nafasi za ajira kwa kutoa fursa takribani 1,500 kwa Uingereza pekee na kwamba mpango huo ni muhimu nchi husika.

Mkataba huo umesainiwa katika mkutano wa pamoja kati ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron na Rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy mjini Paris nchini Ufaransa.

Rais Sarkozy anakabiliwa na kipute cha kuwania urais nchini Ufaransa Mwezi Aprili na Mei mwaka huu ambapo tayari ameshatangaza kuwania nafasi hiyo.

Viongozi hao hawakusita kuzungumzia hali ya mambo nchini Syria na wamesema ni lazima lifanyike lolote linalowezekana ili kukomesha mauaji nchini Syria.

Wametoa wito kwa dunia kuunganisha nguvu ili kuhakikisha suluhu ya kudumu inapatikana nchini Syria

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.