Pata taarifa kuu
Palestina-Marekani

Shinikizo zaidi laongezeka kupata taifa huru la Palestina, Marekani yapania kutumia kura yake ya turufu

Wakati ajenda ya nchi ya Palestina kupatiwa uanachama wa kudumu katika baraza la Umoja wa Mataifa ikiendelea kuungwa mkono na mataifa ya kiarabu, nchi ya Marekani imeendelea kushikilia msimamo wa kutopiga kura yake kuitambua Palestina kama taifa huru.

گMahmoud Abbas, Khaled Meshaal, Ba der kati yao
گMahmoud Abbas, Khaled Meshaal, Ba der kati yao RFI
Matangazo ya kibiashara

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Hillary Clinton, amesema jambo hilo lisichukuliwe kwa haraka na kwamba ni lazima kwanza mgogoro katika eneo la Gaza utatuliwe kwanza ndio Palestina ianze harakati hizo.

Nae msemaji wa waziri mkuu wa Israel, Mark Regev amesema kuwa nchi yake haitishwi na Palestina wala nchi yoyote na hata Umoja wa Mataifa kuhusu kutoitambua nchi ya Palestina na itaendelea na mpango wake wa kuendelea makazi ya kudumu katika eneo la mashariki.
 

 

 

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.