Pakistani-Marekani
Ujumbe ulio rekodiwa wa Bin Laden wapongeza harakati za mabadiliko katika nchi za kiarabu
Mtandao wa Al Qaeda umetoa mkanda wa sauti uliorekodiwa kabla ya kifo cha kiongozi wake Osama Bin Laden ambaye alitowa ujumbe mzito wa kusifia mabadiliko ya utawala ambayo yalifanyika katika nchi za misri na Tunisia.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kanda ya sauti ikiwa na urefu wa dakika kumi ns mbili na sekunde thelathini na saba imebeba ujumbe wa kuyahamasisha mataifa mengine ya kiarabu ambayo yapo chini ya utawala mbovu kufanya mabadiliko.
Osama hakuishia hapo bali aliwataka wanamapinduzi kuharakisha juhudi zao kwa kuwa wakichelewa huenda wakakosa kabisa haki ambayo wanastahili kuipata kutoka kwa madhalimu yanayoongoza mataifa hayo.