Shambulio la Taliban laua watu 36
Takribani watu thelathini na sita wameuwawa na wengine ishirini wamejeruhiwa katika mapigano baina ya wanamgambo wa Taliban na wafanyakazi wa kampuni moja ya ujenzi ,mapigano yaliyodumu kwa saa kadhaa.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Tukio hilo limetokea mashariki mwa jimbo la Paktia karibu na mpaka wa Pakistan majira ya saa nane usiku kwa saa za Afghanstani.
Shambulio hilo ni baya zaidi kutokea baada ya tukio lililotokea mwezi February mwaka huu ambapo Taliban ilishambulia Benki moja katika eneo la jalalabad na kusababisha vifo vya watu thelathini na wanane wakiwemo maafisa wa polisi waliokuwa wakichukua mishahara yao.
Mkurugenzi wa kampuni ya Galaxy Sky ambayo wafanyakazi wake wameuwawa ameliambia shirika la habari la Ufaransa kuwa hafahamu chanzo cha wafanyakazi wake kushambuliwa.
Taliban imekuwa ikikwamisha mipango mbalimbali ya serikali ya Afghanstani ikiwa ni harakati za kuupunguzia uwezo uongozi wa rais Hamid Karzai na mara kwa mara wamekuwa wakiwateka wafanyakazi wa kigeni.