Pata taarifa kuu

Mvua kubwa yasababisha maafa Beijing, China

Nairobi – Karibia watu 11 wamefariki wakati wengine 27 hawajulikani waliko baada ya mvua kubwa inayoendelea kunyesha jijini Beijing nchini China kusababisha mafuriko na uharibifu wa miundo mbinu.

Rais wa China Xi Jinping, ametoa wito wa kufanyika kwa "kila juhudi" kuokoa watu "walionaswa" kwenye matope
Rais wa China Xi Jinping, ametoa wito wa kufanyika kwa "kila juhudi" kuokoa watu "walionaswa" kwenye matope AP - Andy Wong
Matangazo ya kibiashara

Miongoni mwa watu waliofariki ni wafanyikazi wawili wa uokoaji walioangamia wakati wakiwa kazini kutoa huduma za msaada.

Zaidi ya watu laki moja kwenye jiji hilo ambao walikuwa wanakabiliwa na hatari ya kuathiriwa na mafuriko wamehamishwa katika maeneo salama.

Baadhi ya barabara zimeonekana kuharibiwa na mafuriko yaliosababishwa na mvua hiyo wakati huu maofisa wa uokoaji wakiendelea na shughuli za kuwatafuta watu wanaohofiwa kuwa huenda wamefunikwa na udongo.

Karibia watu 11 wamefariki wakati wengine 27 hawajulikani waliko baada ya mvua kubwa inayoendelea kunyesha jijini Beijing
Karibia watu 11 wamefariki wakati wengine 27 hawajulikani waliko baada ya mvua kubwa inayoendelea kunyesha jijini Beijing via REUTERS - CHINA DAILY

Rais wa China Xi Jinping, ametoa wito wa kufanyika kwa "kila juhudi" kuokoa watu "walionaswa" kwenye matope baada ya mvua kubwa kunyesha katika maeneo ya kaskazini mwa nchi, vyombo vya habari vya serikali vimeripoti.

Mamlaka za mitaa "lazima zifanye kazi nzuri katika kutibu waliojeruhiwa na kufariji familia za wahasiriwa, na kupunguza majeruhi", CCTV ilimnukuu Xi akisema.

Serikali imesema inawahamisha watu walio katika maeneo hatari
Serikali imesema inawahamisha watu walio katika maeneo hatari AFP - STR

Picha za moja kwa moja kutoka kwa kituo cha utangazaji cha CCTV Jumanne asubuhi zilionyesha baadhi ya mabasi yakiwa yamezama kwenye maji ya mafuriko katika kitongoji cha Beijing kusini magharibi mwa Fangshan.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.