Pata taarifa kuu

Watu 22 wamefariki katika mafuriko Korea kusini

Takriban watu 22 wamefariki na wengine 14 hawajulikani walipo baada ya mvua kubwa kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi nchini Korea Kusini wakati huu maelfu ya wengine wakitakiwa  kuhama makazi yao.

Inahofiwa kuwa huenda idadi ya waliofariki ikaongezeka
Inahofiwa kuwa huenda idadi ya waliofariki ikaongezeka via REUTERS - YONHAP
Matangazo ya kibiashara

Mvua kubwa imekuwa ikinyesha nchini humo kwa kipindi cha siku tatu zilizopita, na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi hali ambayo imechangia kufurika kwa bwawa kubwa.

Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya ndani nchini humo, watu 22 wameuawa na wengine 14 hawajulikani walipo kutokana  mvua hiyo kubwa, wengi wao wakiwa wamezikwa na maporomoko ya ardhi wengine wakiripotiwa kuanguka kwenye bwawa lililofurika.

Mamlaka nchini humo inasema watu 22 wamefariki katika maporomoko ya udongo na mafuriko
Mamlaka nchini humo inasema watu 22 wamefariki katika maporomoko ya udongo na mafuriko © REUTERS

Shirika la habari la Yonhap la Korea Kusini lilikuwa limeripoti awali vifo 24, likiwanukuu maafisa wa shirika la kutoa misaada.

Zaidi ya wakaazi 6,400 katika kaunti ya kati ya Goesan wameombwa kuhama makazi yao baada ya bwawa la Goesan kuaanza kufurika.

Waokoaji wanaendelea na shughuli za kuwatafuta watu waliofunikwa na udongo
Waokoaji wanaendelea na shughuli za kuwatafuta watu waliofunikwa na udongo via REUTERS - YONHAP NEWS AGENCY

Baadhi ya watu ambao wameripotiwa kutoweka walisombwa na maji wakati mto ulipofurika katika jimbo la Gyeongsang Kaskazini, wizara hiyo ilisema.

Idadi ya vifo inatarajiwa kuongezeka wakati mashirika ya serikali ya mitaa yanatathmini uharibifu huo kote nchini.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.