Watu wanne kushtakiwa kwa kuiangusha ndege ya Malaysia mwaka 2014
Washukiwa wanne, wanaominiwa kuhusika na kuiangusha ndege ya abiria ya Malaysia MH17 mwaka 2014 nchini Ukraine, wametajwa na watafunguliwa mashtaka.
Imechapishwa:
Raia watatu wa Urusi, na mmoja wa Ukraine, watafunguliwa mashataka ya kusafirisha kombora lililosababisha kuiangusha ndege hiyo na kusababisha vifo vya watu 298.
Ndege hiyo ya abiria ilikuwa imetokea mjini Amsterdam nchini Uholanzi kwenda nchini Kuala Lumpur, wakati ilipoangushwa katika angaa la Mashariki mwa Ukraine wakati wa mzozo kati ya nchi hiyo na Urusi.
Wanne hao ambao wametajwa kuwa Igor Girkin, Sergey Dubinskiy na Oleg Pulatov wote raia wa Urusi na Leonid Kharchenko kutoka Ukraine, watafikishwa Mahakamani nchini Uholanzi kuanzia tarehe 9 mwezi Machi mwaka 2020.
Hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa washukiwa hao imetangazwa.