Pata taarifa kuu
INDONESIA-SIASA-UCHAGUZI

Uchaguzi wa urais Indonesia: Widodo aongoza lkwa kura nyingi

Rais anaye maliza muda wake nchini Indonesia, Joko Widodo, anaonekana kuwa atashinda uchaguzi wa urais uliyofanyika leo Jumatano Aprili 17, 2019.

Wagombea wawili katika uchaguzi wa urais indonesia, (kushoto) rais anayemaliza muda wake, Joko Windodo na Prabowo Subianto wakati wa kampeni ya uchaguzi.
Wagombea wawili katika uchaguzi wa urais indonesia, (kushoto) rais anayemaliza muda wake, Joko Windodo na Prabowo Subianto wakati wa kampeni ya uchaguzi. ©REUTERS/Willy Kurniawan - Montage RFI
Matangazo ya kibiashara

Joko widodo anaongoza kwa 54.7% ya kura hadi 55.7% kupitia mfumo wa kuhesabu haraka kwa jumla ya 55% hadi 78 ya kura ambazo zimekwisha hesabiwa.

Hata hivyo, Philips Vermonte, Mkurugenzi wa taasisi ya CSIS, inayofuatilia kwa karibu uchaguzi huo, ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba ni mapema kutangaza mshindi wa uchaguzi huo.

Kambi ya Prabowo pia imetoa wito kwa wafuasi wake kuwa na uvumilivu. "Tutasubiri," amesema msemaji wa kampeni ya Prabowo Subianto, Dahnil Anzar Simanjuntak, akibainisha kwamba bado ni mapema kumjuwa mshindi.

Zaidi ya raia milioni 192 wa Indonesia wamepiga kura Jumatano hii kumchagua rais wao na wabunge baada ya kampeni iliyodumu miezi sita, ambayo ilitawaliwa na masuala ya kiuchumi na kuongezeka kwa ushawishi wa Uislam wa kihafidhina.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.